Breaking

Showing posts with label launeyempire..... Show all posts
Showing posts with label launeyempire..... Show all posts
July 18, 2017

Jamani Mwenzenu Demu Wangu ni Mjeuri, Anakiburi na Mkaidi Sana Nimfanyeje?

Wana Udaku naombeni msaada kwa huyu mdada sijui ata nini nimfanyie anakiburi na mjeuri ajabu akiambiwa tofauti na alivyotegemea ananuna wenda ata asiongee ama kama tunaongea kwa simu anakata na hapokei simu, nikimwambia nitamwacha analia na kulalamika eti nimepata mtu mwingine na ndiyo maana nimeamua kumwachaa,,,, kiukweli mimi ni mwaminifu ila sasa anaifanya niamini msemo ambao mwalimu wangu aliniambia nikiwa form two kwamba kuwa na demu mmoja unatafuta uginjwa wa moyo....kiukweli namppenda san na ndiyo maana sijaribu ata kumchiti ila sasa natamani ata ajikoze mdada mwenye kuhitaji mume tuendelee maana sasa inatosha naumia kiukweli acheni masihara kwa mapenzi yanauma kuliko kuchapwa mboko sure....msaada ata kama kuna mdada ambaye yupo siriasi naomba aje tujenge mahusiano ya kweli mimi naweza kumilikiwa bila ata kusumbua love you wanajamiii mnanielimisha mengi sana!

July 15, 2017

Hiki Ndicho Kinachoitwa Kichaa Cha Mapenzi

Kabla mtu hajaoa au kuolewa , huamini kabisa kwamba, kabla hajafanya mapenzi au tendo la ndoa na mtu anayemwita mpenzi wake, bado hawezi kudai kwamba, huyo mtu ni mpenzi wake na kwajibika kwake kama mpenzi.

Vijana wengi huamini kwamba, baada ya kukutana kimwili, ndipo wanaweza kudai kwamba, hao ni wapenzi wao na kwamba kukutana kimwili, ndiyo mapenzi au kupenda kwenyewe.

Inapotokea wanapokutana huvutiwa na tendo la ndoa, huamini kabisa kwamba, uhusiano nao utakuwa mzuri. Kwao, tendo la ndoa ndio kipimo cha uimara wa uhusiano wao.

Baada ya kufanya mapenzi, wapenzi hao huamini kwamba, sasa wanaweza kujitolea kwenye uhusiano huo na kwamba, wanaweza kuwa na nguvu nao kwa asilimia kubwa.

Suala hili, kuna wataalamu huliita mtego wa kimapenzi. Huitwa hivyo, kwa sababu huwafanya wapenzi kutokuangalia sifa nyingine na badala yake kuweka nguvu kwenye mwili, yaani tendo la ndoa.

Upofu hutokea kutokana na kuzalishwa kwa kemikali nyigi mwilini, zenye kumfanya mtu asiweze kujiuliza kuhusu maeneo mengine ya kimasha ya binadamu, zaidi  ya mwili.

Kinachotokea ni mwili kuvutwa na wale tunaowapenda kwa kuzalisha homoni inayofahamika kama ‘phenylethylamine’ au PEA kwa kifupi.

Kemikali au homoni hii pamoja na nyingine kama vile ‘depomine’ na ‘norepinephrine’ (ambazo huchochea hali za kimwili) na ‘ testosterone’(ambayo huongeza hamu ya kujaamiana), huzalishwa mara baada ya kukutana kimwili.

Baada ya kuzaliswa kwa homoni hizi, akili ya mtu huona mwili tu, yaani mapenzi na siyo sifa nyingine. Hapa ndipo ambapo, mtu hujikuta hawezi kujizuia tena kukutana kimwili na mpenzi wake, mara baada ya kukutana naye mara ya moja.

Baada ya kufanya mapenzi na kufikia kileleni, huzalishwa homoni iitwayo ‘oxytocin’ (ambayo huhusika na mihemiko), homoni hii humfanya mtu kujikuta anapenda kuwa karibu na kujifungamanisha na mtu aliyefanya naye mapenzi. Tunaweza kusema, ukaribu kwa wapenzi wawili huongezeka na unakuwa ni ukaribu wa mwili zaidi.

Kuzalishwa kwa homoni hizi, ni jambo ambalo mtu hawezi kulizuia na huwa linakuja kwa nguvu sana, kiasi kwamba, mtu kuwa kama amepoteza ufahamu wa maeneo mengineyo ya kimaisha isipokuwa mapenzi tu.

Homoni hizi humfanya mtu kuwa na hisia za kuvutiwa na mwingine, uchangamfu, ukaribu, kuvutiwa na hisia za ukamilifu zaidi. Wale waliowahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi kabla ya ndoa au wale waliowahi au wanaotoka nje ya ndoa zao kwa kuvutwa kimwili na wapenzi wengine, wanajua inavyokuwa.

Lakini homoni hizi, hatimaye huanza kupungua na mtu huanza kuhisi kwamba alikosea. Huoni tena na huhisi kama ilivyokuwa awali. Sasa haoni kuwa mpenzi wake ni mzuri au anafaa kama iivyokuwa awali. Kwa sababu, homoni zile zimeshuka sana, mwili unakuwa hauna maana tena.

Kwa bahati mbaya  kile kilichokuwa kinaitwa upendo, kilikuwa kimefungiwa kwenye mwili na homoni hizo ambazo kwa sasa hazipo. Hivyo, wapenzi hawana kingine cha kushika ambacho, wataweza kukiita mapenzi.

Unajua sasa ni kwa nini, tangu kale kabisa suala la wachumba kukutana kimwili kabla ya ndoa lilikuwa likipingwa sana? ni kwamba, watu wanapokutana kimwili, uwezo wa kukaguana tabia unakuwa umefungwa kutokana na kufumuka kwa homoni hizi, ambazo hubadili hali ya mtu na hisia zake kwa ujumla.

Kwa nini unadhani watu, hasa wanaume wakishaanza mapenzi ya kimwili na mtu mpya, yaani nyumba ndogo au yeyote, inakuwa rahisi sana kwao kujisahau na kukamatwa? Sababu ni hiyo hiyo, kwamba, uzalishwaji wa homoni hizi huwa ni mkubwa kiasi cha mtu kuamini kwamba, hakuna kingine chene kufurahisha na kuliwaza kama uhusiano huo.

Kumbuka, watu wawili wanapovutana, kwa maneno mengine tunasema kuna kemia kati yao. Hii ina maana kwamba, huwa kuna mabadiliko ya badhi ya homoni kama nilivyosema. Lakini,

wanapokutana, homoni hizi huwa nyingi kiasi cha kufanya upofu wa muda. Unaweza kuwa upofu wa mwezi, mwaka au miaka.

Upofu huu unapmalizika, uhusianao huwa ni wa vurugu tupu, kwa sababu kama nilivyosema awali, hqakuna mahali pengine pa kushika  siyo tabia, mienenfo waa haiba.

Upofu huu unapomalizika, uhusiano huwa ni wa vurugu tupu, kwa sababu kama nilivyosema awali, hakuna mahali pengine pa kushika siyo tabia, mienendo wala haiba.

Inashauriwa kwamba, mtu anapovutiwa na mwingine au watu wanapovutana ni vema wakawa wangalifu sana. kwanza, wajue kwamba, uhusino ambao msingi wake ni miili tu, yaani tendo la ndoa haudumu, kwani homoni zitokanazo na kukutana watu kimwili, hazina maisha, huwa zinaisha haraka.

Lakini pia inashauriwa kwamba, mtu anapoingia kwenye mapenzi ajaribu kushariana au kuukagua moyo wake, akili pamoja na hisia zake. Kuacha tu mabadiliko ya hali ya mwili yakatawala ni kutafuta maumivu.

Hebu jiulize, ni kwa nini mapenzi yanapoanza kwa moto sana, huzimika haraka  au kwa kishindo sana? ni kwa sababu yanajengwa kwenye msingi usioaminika, yaani katika mihemiko na kimapenzi. Penzi linalokua polepole ndilo lenye kushika, kwani halina msingi wa mwili.

July 14, 2017

Hizi Ndizo Sababu za Lulu Kupungua


MSANII kutoka Bongo Muvi, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwa mara ya kwanza amefungukia sababu zinazomfanya kupungua sana mwili kuwa ni kushinda kwa kula matunda pamoja na mazoezi makali ya viungo.
Akizungumza na Star Mix, Lulu alisema kuwa, ameamua kupunguza mwili kwa makusudi na kwamba kila siku anashinda akila matunda na kufanya mazoezi magumu ya viungo.
“Watashangaa sana kuniona napungua lakini nafanya hivi wala sijashauriwa na mtu ni kuweka tu mwili wangu sawa. Nafanya sana mazoezi, naenda gym kila siku na kuhakikisha muda mwingi nashinda kwa kula matunda kuliko chakula,” alisema Lulu.
Wiki mbili zilizopita, Lulu alizua gumzo katika Ukumbi wa King Solomon, Namanga jijini Dar baada ya kuonekana akiwa amepungua tofauti na zamani.
July 14, 2017

Rufaa Vyeti Feki: 600 Wagonga Mwamba, 450 Warudishwa Kazini



Watumishi wa umma 450 walioondolewa kazini kutokana na kudaiwa kutumia vyeti vya kughushi wamerudishwa kazini baada ya kushinda rufaa zao.

Baada ya kutangazwa kwa Orodha ya watumishi wenye vyeti feki, 1050 walikata Rufaa huku  8800 wakiridhika na matokeo hayo.

Mbali na hilo, Serikali imesitisha mishahara kwa watumishi wa umma ambao walitakiwa kuwasilisha vyeti vyao kwa uhakiki lakini mpaka sasa hawajafanya hivyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk.Laurean Ndumbalo alisema watumishi hao wameshinda rufaa zao hivyo wataandikiwa barua za kurudishwa katika utumishi wa umma.

Alisema katika rufaa hizo, wengi walikuwa wanawake walioolewa na kubadili majina yao kwa kutumia ya waume zao.

“Kuna baadhi walitumia majina mawili alipokuwa kidato cha nne baadaye alilazimika kutumia matatu na kusababisha mkanganyiko hivyo tumejiridhisha na wanarudishwa katika utumishi wa umma,” alisema Dk. Ndumbalo.

Alisema Serikali pia imesitisha mishahara kwa watumishi wa umma ambao walitakiwa kuwasilisha vyeti vyao kwa uhakiki lakini mpaka sasa hawajafanya hivyo.

“Serikali imesitisha mishahara ya watumishi wote ambao muundo wa utumishi wao uliwataka kuwa na sifa ya kufaulu kidato cha nne wakati wanaajiriwa lakini hawakuwasilisha vyeti vyao kuhakikiwa na Baraza la Mitihani.

“Tunasitisha mishahara yao kuanzia mwezi Julai hadi hapo watakapowasilisha vyeti vyao kuhakikiwa,” alisema Dk. Ndumbalo.

Dk. Ndumbalo aliongeza kuwa kwa watumishi walioajiriwa wakiwa darasa la saba kabla ya waraka wa Utumishi wa Umma namba moja wa mwaka 2004 uliowataka waajiriwa kuwa na sifa ya kidato cha nne, wataendelea na kazi mpaka watakapostaafu.

Alisema sera ya Menejimenti na Ajira katika utumishi wa umma toleo la mwaka 1998 lilianza kutekelezwa Mei 20, 2004 hivyo kwa walioajiriwa kabla ya hapo warudishwe kazini kama waliondolewa kimakosa.

“Nasisitiza kuwa watumishi wote wa umma walioajiriwa kwa sifa ya elimu ya darasa la saba kabla ya Mei 20 hawahusiki na uhakiki wa vyeti vya kufaulu mtihani wa kidato cha nne na wataendelea kuwa watumishi wa umma katika vyeo vyao mpaka watakapostaafu kazi,” alisema Dk.Ndumbalo.

Aidha alisema serikali inatangaza ajira mpya 10,184 katika sekta mbalimbali huku ikitoa ajira 3,172 kwa sekta ya afya.

July 14, 2017

Kimenuka...Machangudoa Waundiwa Vikundi vya Ulinzi Moshi

 Wananchi wa Kata ya Mawenzi, Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, wamelazimika kuunda vikundi vya ulinzi katika mitaa yao nyakati za usiku kwa lengo la kutokomeza biashara ya uchanguduo na uhalifu uliokithiri katika kata hiyo.

Hayo yamebainishwa na wananchi hao katika mkutano uliotishwa na diwani wa kata hiyo, Hawa Mushi, kwa lengo la kujadili changamoto zinazowakabili katika maeneo yao na kutoa maazimio.

Janeth Mbwambo, mkazi wa eneo hilo, amesema tatizo la machangudoa kuzagaa katika maeneo ya kata hiyo limekuwa kero nyakati za usiku pamoja na vijana wanaofanya uhalifu pia wamesababisha watu kuwa na hofu ya usalama wao.

Mkazi wa kata hiyo, Mary William, amesema pamoja na juhudi zinazofanywa za kuimarisha ulinzi bado hali imekuwa mbaya kwa kata yao huku akidai kuwa kama hawataimarisha ulinzi wao wenyewe tatizo hilo litaendelea kuwepo.

Diwani wa kata hiyo amesema wamejitahidi kupambana na uhalifu na machangudoa lakini bado tatizo limekuwa likiendelea na kwamba wataingia katika ulinzi wenyewe ili kukomesha kabisa jambo hilo.

“Tunaingia katika mapambano wenyewe ili kuwakabili machangudoa pamoja na  uhalifu unaofanywa na watu kutoka nje ya kata yetu na si wakazi wa eneo husika, hali hiyo imeichafua sana kata yetu,” amesema Diwani Mushi.

Akijibu kero za wananchi hao kuhusu kelele za mziki nyakati za usiku, Meya wa Manispaa ya Moshi, Raymond Mboya amesema suala hilo limeshatolewa maelekezo kwa mkurugenzi wa manispaa hiyo.

Amesema kama mtu hataweza kufuata masharti ya kupiga muziki usiku, vyombo vyake vya muziki vitachukuliwa na kupelekwa katika halmashauri hiyo na akiendelea kukaidi atafungiwa na faini yake ni kiasi cha Sh.1 Millioni.

Akizungumzia suala la wafanyabiashara maarufu kama wamachinga Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini, Jaffar Michael, amesema suala lao limeshapitishwa bungeni kwamba ili waweze kutambulika wanatakiwa kila mmoja ajisajili.

Amesema jambo hilo litasaidia kuepusha migongano na itawaepushia kufukuzwa na kupigwa na baadhi ya mgambo, na sheria hiyo inatakiwa ianze Julai Mosi mwaka huu kwani watakuwa wanatambulika kisheria.

July 14, 2017

Kimenuka...Machangudoa Waundiwa Vikundi vya Ulinzi Moshi

 Wananchi wa Kata ya Mawenzi, Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, wamelazimika kuunda vikundi vya ulinzi katika mitaa yao nyakati za usiku kwa lengo la kutokomeza biashara ya uchanguduo na uhalifu uliokithiri katika kata hiyo.

Hayo yamebainishwa na wananchi hao katika mkutano uliotishwa na diwani wa kata hiyo, Hawa Mushi, kwa lengo la kujadili changamoto zinazowakabili katika maeneo yao na kutoa maazimio.

Janeth Mbwambo, mkazi wa eneo hilo, amesema tatizo la machangudoa kuzagaa katika maeneo ya kata hiyo limekuwa kero nyakati za usiku pamoja na vijana wanaofanya uhalifu pia wamesababisha watu kuwa na hofu ya usalama wao.

Mkazi wa kata hiyo, Mary William, amesema pamoja na juhudi zinazofanywa za kuimarisha ulinzi bado hali imekuwa mbaya kwa kata yao huku akidai kuwa kama hawataimarisha ulinzi wao wenyewe tatizo hilo litaendelea kuwepo.

Diwani wa kata hiyo amesema wamejitahidi kupambana na uhalifu na machangudoa lakini bado tatizo limekuwa likiendelea na kwamba wataingia katika ulinzi wenyewe ili kukomesha kabisa jambo hilo.

“Tunaingia katika mapambano wenyewe ili kuwakabili machangudoa pamoja na  uhalifu unaofanywa na watu kutoka nje ya kata yetu na si wakazi wa eneo husika, hali hiyo imeichafua sana kata yetu,” amesema Diwani Mushi.

Akijibu kero za wananchi hao kuhusu kelele za mziki nyakati za usiku, Meya wa Manispaa ya Moshi, Raymond Mboya amesema suala hilo limeshatolewa maelekezo kwa mkurugenzi wa manispaa hiyo.

Amesema kama mtu hataweza kufuata masharti ya kupiga muziki usiku, vyombo vyake vya muziki vitachukuliwa na kupelekwa katika halmashauri hiyo na akiendelea kukaidi atafungiwa na faini yake ni kiasi cha Sh.1 Millioni.

Akizungumzia suala la wafanyabiashara maarufu kama wamachinga Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini, Jaffar Michael, amesema suala lao limeshapitishwa bungeni kwamba ili waweze kutambulika wanatakiwa kila mmoja ajisajili.

Amesema jambo hilo litasaidia kuepusha migongano na itawaepushia kufukuzwa na kupigwa na baadhi ya mgambo, na sheria hiyo inatakiwa ianze Julai Mosi mwaka huu kwani watakuwa wanatambulika kisheria.

July 14, 2017

ACACIA Yakubali Kulipa mirabaha iliyowekwa katika sheria mpya ya madini

Kufuatia mabadiliko yaliyofanywa na Bunge katika sheria za usimamizi wa rasilimali nchini, ongezeko la mrabaha unaotarajiwa kulipwa serikali uliongezeka kutoka katika asilimia 4 iliyokuwa katika sheria za zamani.

Katika kuonyesha kukubaliana na mabadiliko hayo, Kampuni ya uchimbaji madini nchini ya Acacia imekubali kuilipa serikali mrabaha wa asilimia 6 unaoendana na sheria mpya zilizoanza kutumika mwezi huu mwanzoni baada ya kusainiwa na Rais Julai 5.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo leo inaeleza kuwa, ili kuepuka mkanganyiko au mvurugano zaidi kwenye kazi zao katika siku za usoni, watatimiza matakwa yanayohitajika katika ongezeko la mrabaha wa katika madini ya dhahabu, fedha na shaba la asilimia 6

==>Isome taarifa ya ACACIA hapo chini

July 14, 2017

ACACIA Yakubali Kulipa mirabaha iliyowekwa katika sheria mpya ya madini

Kufuatia mabadiliko yaliyofanywa na Bunge katika sheria za usimamizi wa rasilimali nchini, ongezeko la mrabaha unaotarajiwa kulipwa serikali uliongezeka kutoka katika asilimia 4 iliyokuwa katika sheria za zamani.

Katika kuonyesha kukubaliana na mabadiliko hayo, Kampuni ya uchimbaji madini nchini ya Acacia imekubali kuilipa serikali mrabaha wa asilimia 6 unaoendana na sheria mpya zilizoanza kutumika mwezi huu mwanzoni baada ya kusainiwa na Rais Julai 5.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo leo inaeleza kuwa, ili kuepuka mkanganyiko au mvurugano zaidi kwenye kazi zao katika siku za usoni, watatimiza matakwa yanayohitajika katika ongezeko la mrabaha wa katika madini ya dhahabu, fedha na shaba la asilimia 6

==>Isome taarifa ya ACACIA hapo chini

July 14, 2017

Mume Hafiki Kileleni ni Kawaida au Matatizo?

Habari zenu wapendwa, Weekend nilipata mgeni ambae ni ndugu yangu, ameolewa ana miezi 3 tu, lililomleta hasa ni kutafuta ufumbuzi anasema tangia ameolewa Mume wake alifika kileleni siku ya Honey Moon tu wana miezi 3 sasahivi hajawai fika tena lakini akiingia uwanjani anaweza ata kukesha tatizo ni hilo hafiki mwisho, amemuuliza kwanini anasema nayeye hajui kwanini, nimeona niwaletee nyinyi wana JF mabingwa wa TIBA ya kila tatizo, maana mdogo wangu amekosa amani ameshaanza kuona kupata watoto itakuwa ndoto

July 14, 2017

Mume Hafiki Kileleni ni Kawaida au Matatizo?

Habari zenu wapendwa, Weekend nilipata mgeni ambae ni ndugu yangu, ameolewa ana miezi 3 tu, lililomleta hasa ni kutafuta ufumbuzi anasema tangia ameolewa Mume wake alifika kileleni siku ya Honey Moon tu wana miezi 3 sasahivi hajawai fika tena lakini akiingia uwanjani anaweza ata kukesha tatizo ni hilo hafiki mwisho, amemuuliza kwanini anasema nayeye hajui kwanini, nimeona niwaletee nyinyi wana JF mabingwa wa TIBA ya kila tatizo, maana mdogo wangu amekosa amani ameshaanza kuona kupata watoto itakuwa ndoto

July 14, 2017

Hakuna Msalie Mtume....Vituo vya Mafuta Kuendelea Kufungwa

Vituo kadhaa vya kuuza  dizeli, petroli na mafuta ya taa vimefungwa jijini hapa kutokana na kutokuwa na mashine za kielektroniki za kutoa risiti (EFDs).

Hatua hiyo inayotekelezwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imeelezwa kuwaathiri si tu wenye vituo bali hata watumiaji.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo amesema leo  Julai 14 na kuongeza kwamba  wanaendelea na kazi hiyo nchi nzima ili kuhakikisha sheria inatekelezwa.

July 14, 2017

Hakuna Msalie Mtume....Vituo vya Mafuta Kuendelea Kufungwa

Vituo kadhaa vya kuuza  dizeli, petroli na mafuta ya taa vimefungwa jijini hapa kutokana na kutokuwa na mashine za kielektroniki za kutoa risiti (EFDs).

Hatua hiyo inayotekelezwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imeelezwa kuwaathiri si tu wenye vituo bali hata watumiaji.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo amesema leo  Julai 14 na kuongeza kwamba  wanaendelea na kazi hiyo nchi nzima ili kuhakikisha sheria inatekelezwa.

July 14, 2017

Serikali kuiunganisha mikoa ya Rukwa na Songwe

Serikali imesema kuwa itaanza kujenga daraja la Mto Momba litakaloiunganisha Mikoa ya Rukwa na Songwe kwaajili ya kuondoa kero kwa wananchi ambayo imekuwa ikiwasumbua hasa wakati wa masika.

Hayo yamesemwa Naibu waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani mara baada ya ziara ya ukaguzi wa barabara Kasansa mpaka Kilyamatundu ambapo amesema kuwa tayari Serikali imeshampata mkandarasi atakayejenga daraja hilo.

“Serikali imeshatoa kiasi cha sh. Bilioni tatu  fedha hizo zimetusaidia kutangaza zabuni na kumpata mkandarasi, tayari Mkandarasi wa ujenzi huu ameshapatikana na mkataba wa makubaliano ya ujenzi umeshakamilika hivyo mkandarasi atausaini rasmi hivi karibuni,” amesema Eng. Ngonyani.

Aidha, Eng.Ngonyani amesema kuwa ujenzi na kukamilika kwa daraja hilo kutasaidia kukuza uchumi na wa wananchi wa mikoa hiyo, hivyo kuongeza pato la taifa wakati huu nchi inaelekea kwenye uchumi wa kati wa Viwanda

Vile Vile amemuagiza Meneja Wa Wakala wa barabara (TANROADS) Mkoa wa Rukwa kuhakikisha anatoa ajira kwa wakazi waliopo kata ya Kipeta ambapo ujenzi wa daraja hilo utafanyika.

Hata hivyo, kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kwela, Ignas Malocha ameishukuru Serikali ya awamu ya tano ya Dkt. John Magufuli kwa kutekeleza ahadi ya ujenzi wa daraja hilo ambalo kukamilika kwake kutawaletea maendeleo wakazi hao kwa vile litaufungua Mkoa wa Rukwa na kuunganisha na Songwe na Katavi.

Naye meneja wa TANROADS Rukwa Eng. Msuka Mkina amewahakikishia wakazi kijiji cha  Kilyamatundu kuwa Wakala utasimamia ujenzi huo ili ukamilike kwa wakati na viwango na kupitia mradi huo wananchi hao watapata ajira.

July 14, 2017

Hakuna Msalie Mtume....Vituo vya Mafuta Kuendelea Kufungwa

Vituo kadhaa vya kuuza  dizeli, petroli na mafuta ya taa vimefungwa jijini hapa kutokana na kutokuwa na mashine za kielektroniki za kutoa risiti (EFDs).

Hatua hiyo inayotekelezwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imeelezwa kuwaathiri si tu wenye vituo bali hata watumiaji.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRA, Richard Kayombo amesema leo  Julai 14 na kuongeza kwamba  wanaendelea na kazi hiyo nchi nzima ili kuhakikisha sheria inatekelezwa.

July 14, 2017

Baraka The Prince Amkana Katu Katu Ali Kiba......

Msanii Baraka The Prince ambaye yupo chini ya usimamizi wa kampuni ya RockStar4000 amefunguka na kusema kuwa yeye ni msanii aliye chini ya usimamizi wa RockStar4000 na si msanii aliye chini ya Alikiba.

Baraka The Prince amesema hayo kupitia kipindi cha 5 Selekt na kusema yeye anatambua kuwa Alikiba sasa amekuwa Director wa kampuni hiyo na anaamini anaweza kufanya vizuri lakini yeye hana taarifa zozote juu ya mchongo huo ambao ameupata Alikiba kwenye uongozii wake huo.

"Mimi sitaki sana kuzungumzia sana juu ya Alikiba kuwa Director wa RockStar4000 kwani kipindi ambacho yeye anaingia mikataba mimi nilikuwa Nairobi na wao walikuwa Afrika Kusini na sijapata nafasi kusikia chochote hivyo kwa sasa bado sijui vizuri hilo jambo, siwezi kulizungumzia japo nafahamu maana naweza kuzungumzia nikazungumza nikasema jambo lisilo la kweli. Ila nimefurahi sababu Alikiba ni kaka yangu na naishi naye vizuri na najua kuwa kazi itakwenda vizuri". Amesema

Mbali na hilo Baraka The Prince alitoa ufafanuzi kuwa yeye ni msanii anayesimamiwa kazi zake na kampuni ya RockStar4000 na si kusimamiwa na Alikiba kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakidhani au wakihisi hivyo.

"Mimi ni msanii wa RockStar4000 na si msanii wa Alikiba hilo watu naomba waelewe" alisema Baraka The Prince

Kwa kumalizia Baraka The Prince alisema watu wengi wanamchukia kutokana na misimamo yake katika kazi yake ya muziki na kudai wasanii wengi wa bongo wamekuwa wakifanya kazi zao kienyeji sana ndiyo maana anapishana nao, kwani yeye anataka kazi ambayo anashiriki iweze kuwekewa mipango na iende katika viwango.

July 11, 2017

Tafiti: Maji ya Mto Msimbazi yana Sumu

MAJI ya Mtu Msimbazi yamebainika Kuwa yana 'sumu'  ambayo hayawezi kuwa Makazi salama kwa viumbe hai
Serikali imechukua sampuli ya maji ya Mto huo kwa ajili ya kayafanyia Tafititi ili kubaini kiwango cha sumu na ubora wa maji yake kwa matumizi ya binadamu.
Emanuel Gwae, Meneja wa  Maabara ya Mazingira  wa Ofisi ya Mkemia Mkuu, amsema kuwa maji hayo hayana oksijeni ya kiwango cha  milimita3.3  alipokuwa akitoa matokeo ya awali kwa wandishi wa habari leo, 
Amesema  kuwa maji  hayo sio salama kwa viumbe hai
July 09, 2017

MTANZANIA Anayeigiza Kama 'YESU' Asimulia yanayomkuta

Msanii wa kuigiza Ayoub ambaye katika tamthilia ya 'Jambo na vijambo' anaigiza kama Yesu amefunguka na kusema kuigiza kama Yesu katika tamthilia hiyo inamletea shida kwa baadhi ya watu ambao siyo waelewa.
Ayoub alisema hayo alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha eNewz na kudai kuwa kuna wakati hata majirani waligombana na mkewe na hawakutaka kusemeshana naye kwa kuwa mumewe anamuuigiza 'Yesu'
"Hata mke wangu kishagombana na watu kwa sababu tu ya mimi kuigiza kama Yesu, wanamwambia mumewe anamgeza mtume wetu Yesu wetu kwa hiyo usinisemeshe, mke wangu akaja kunipa mimi hizo habari nikabaki kucheka tu, lakini katika ule u serious zaidi sijaona kama kumetokea tatizo kubwa mimi ni muislam lakini yapo makanisa yananiita nikawasaidie kutengeneza kazi ya sanaa baada ya kuniona kwenye kile kipindi, kwa hiyo wenyewe wakristo ambao wamezama kwenye imani kuniona naigiza kama Yesu hawafikirii vibaya sababu hata nachoigiza mle ndani kinaendana na yale aliyokuwa anatenda Yesu, hivyo huwezi kuona amefanya jambo lolote baya yule muhusika wa Yesu ambaye ni mimi" alisema Ayoub
Mbali na hilo Ayoub anasema watu ambao wanakuwa na mtazamo hasi juu ya uhusika wake kama Yesu ni wachache sana ukifananisha na wale ambao wanafurahia kwani mambo mengi ambayo anafanya muhusika ni mambo ya msingi.
"Hata ukiangalia kwenye ukurasa wa facebook wa EATV tukiweka post akitokea mtu ambaye atazungumza vibaya juu ya 'character' Yesu wapo watu wengine wanakuja kumsema sana na kumuelewesha vizuri juu ya uhusika wa Yesu, kwa hiyo utaona watu wanaozungumza uzuri wanashinda kutokana na mazuri ambayo muhusika amefanya" alisema Ayoub
Kipindi cha Jambo na Vijambo kinaruka kila Jumapili kuanzia saa 12:30 jioni katika ting'a namba moja kwa vijana EATV